• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (18 Machi-24 Machi)

    (GMT+08:00) 2017-03-24 18:08:57

    Kenya na Somalia zaahidi kuimarisha mapambano dhidi ya ugaidi

    Rais mpya wa Somalia Mohamed Abdullahi "Farmajo" Mohamed amefanya ziara rasmi ya siku tatu nchini Kenya ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu achaguliwe kuwa rais.

    Alitunukiwa heshima ya kijeshi ya mizinga 21.

    Baadaye yeye na mwenyeji wake Rais Uhuru Kenyatta walifanya mazungumzo kuhusu jinsi ya kuboresha uhusiano kati ya Nairobi na Mogadishu.

    Kenyatta amewaambia waandishi wa habari wamekubaliana kuanzishwa kwa Safari za ndege za moja kwa moja kati ya Nairobi na Mogadishu.

    Aidha waliahidi kuimarisha mapambano dhidi ya ugaidi, kwa kupambana bila huruma na wapiganaji wa kundi la Al-Shabaab, ambao wameongeza mashambulizi ya kigaidi kwenye nchi hizo mbili.

    Kwa upande wake Rais Mohamed ameipongeza Kenya kwa mchango wake mkubwa kwenye mapambano dhidi ya kundi la Al-Shabaab.


    1 2 3 4 5 6 7
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako