Waziri wa Fedha na Mipango, nchini Tanzania Dk Philip Mipango ametaja hatua zinazoendelea kutekelezwa na serikali ili kufikia malengo ya uchumi wa Viwanda.
Maeneo hayo ni kupambana na rushwa, kuimarisha miundombinu ya umeme na barabara.
Dk Mpango amesema pamoja na juhudi hizo, lengo la kufikia uchumi wa Viwanda siyo la serikali pekee.
Dk Mpango aliyasema hayo jijini Dar es salaam wakati wa Warsha ya 22 ya tafiti iliyoandaliwa na Taasisi ya Repoa.
Warsha hiyo inayofanyika kila mwaka, ina lengo la kujadili changamoto, mbinu, uzoefu na jinsi ya kuimarisha taasisi katika malengo ya uchumi wa viwanda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |