Uzalishaji wa Chai nchini Kenya mwaka huu wa 2017 unatarajiwa kushuka kwa asilimia 11 huku chanzo kikuu kikiwa ni ukame ambao ulishuhudiwa kote nchini Kenya. Mamlaka ya kilimo na chakula ya Kenya imesema uzalishaji wa bidhaa hiyo utapungua kutoka kilo milioni 473 zilizoshuhudiwa mwaka jana hadi kilo 420 mwaka huu. Hata hivyo mkuu wa mamlaka hiyo bwana Alfred Busolo amesema bei ya bidhaa hiyo inatarajiwa kuimarika kufuatia kupungua kwa uzalishaji wa bidhaa hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |