• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (8 Mei-12 Mei)

    (GMT+08:00) 2017-05-12 20:31:49

    1-Rais wa Burundi akutana na makamu wa rais wa China

    Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi jana mjini Bujumbura alikutana na makamu wa rais wa China Bw. Li Yuanchao ambaye yuko ziarani nchini humo.

    Kwenye mazungumzo yao, Bw. Li Yuanchao amesema China inapenda kupanua ushirikiano wa kunufaishana na Burundi katika sekta mbalimbali, kuimarisha uaminifu wa kisiasa na kukuza mawasiliano ya kiutamaduni, ili kutia uhai mpya katika uhusiano kati ya nchi hizo mbili.

    Kwa pande wake rais Nkurunziza amesema uhusiano na ushirikiano uliopo kati ya nchi mbili unaendelea vizuri, na kusisitiza kuwa Burundi itaendelea kushikilia sera ya kuwepo wa China moja na kuiunga mkono China katika masuala ya kimataifa ikiwemo suala la Bahari ya kusini ya China na Peninsula ya Korea.


    1  2  3  4  5  6  7  8  9  10  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako