Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Bw. Lu Kang leo hapa Beijing amesema, hivi sasa hali ya Mashariki ya Kati iko katika kipindi muhimu, na China, ikiwa nchi mjumbe wa kudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, itaimarisha ushirikiano na uratibu na nchi za kanda hiyo, na kushirikiana na jumuiya ya kimataifa ili kuhimiza hali ya kanda hiyo ielekee kwenye njia sahihi.
Bw. Lu Kang amesema China inapenda kukuimarisha ushirikiano na nchi za Palestina, Tunisia, Umoja wa Falme za Kiarabu na Qatar na kuhimiza mazungumzo ya amani wakati wa kipindi hiki maalumu. Wakati huo huo, Lu Kang amesema mapendekezo na kanuni zilizotolewa na China kuhusu hali ya Mashariki ya Kati zimekubaliwa na pande mbalimbali husika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |