Rais John Magufuli ameagiza kujengwa uzio katika eneo linalozunguka machimbo ya Tanzanite liliko Simanjiro ikiwa ni hatua yake ya kutaka kukabiliana na utoroshwaji wa rasilimali hiyo.
Amelisisitiza Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kuanza kazi hiyo haraka iwezekanavyo.
Rais Magufuli ambaye yuko ziarani mkoani Manyara amesema vikosi vya ulinzi na usalama vinapaswa kushirikiana kujenga ukuta huo ambao utaanzia eneo la block A hadi D la machimbo hayo.
Baada ya ujenzi huo kukamilika ametaka kufungwa mitambo maalumu ikiwamo kamera zitakazokuwa na uwezo kutambua na kubaini matukio yoyote yanayotendeka katika eneo hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |