Mahakama Kuu ya Kenya imetaja uchakachuaji wa makusudi wa data, na hatua ya tume ya uchaguzi nchini humo kukataa kukubali kuwa walivuruga utangazaji wa matokeo, kuwa ni moja ya sababu zilizofanya majaji wa mahakama hiyo kufuta matokeo ya uchaguzi wa Agosti 8. Jana mahakama kuu ilitoa ufafanuzi wa kina kuhusu uamuzi wake, ambalo umeungwa mkono na kukosolewa na baadhi ya watu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |