Ofisa mmoja wa idara ya ujasusi ya Somalia ameuawa na wengine wawili kujeruhiwa katika mlipuko wa mabomu yaliyotegwa kwenye gari uliotokea jana katika eneo la Bondere mjini Mogadishu.
Polisi aliyekuwepo kwenye eneo la tukio hilo amesema ofisa wa shirika la ujasusi na usalama la Somalia NISA Bw Omar Abu Shine ameuawa kwa mabomu yaliyotegwa kwenye gari lake, na uchunguzi kuhusu kifo chake umeanza.
Wakaazi wamesema ofisa huyo ameuawa akiwa kazini karibu na uwanja wa ndege wa Mogadishu, na kifo chake ni mauaji mapya katika mashambulizi ya kigaidi ya mfululizo yaliyotokea nchini Somalia.
Kundi la Al-Shabaab limetangaza kuhusika na shambulizi hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |