Sudan imesema iko tayari kutoa misaada ya kiufundi kwa Sudan Kusini, kufungua tena visima vyake vya mafuta, vilivyosimamisha uzalishaji kutokana na mapigano. Waziri wa mafuta na gesi wa Sudan Bw. Abdul Rahman Osman amesema hayo alipokutana na mwenzake wa Sudan Kusini Bw. Ezekiel Lol Gatkuoth. Kwa upande wake Bw. Gatkuoth amesema kuongeza uzalishaji wa visima vilivyopo na kufungua visima vilivyofungwa, ni muhimu kwa nchi zote mbili na kunalingana na maslahi ya pande mbili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |