• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rwanda: Rwanda kutoa visa kwa wageni wote pindi wanapoingia

    (GMT+08:00) 2017-11-17 18:51:55

    Serikali ya Rwanda imesema sasa wageni wote wanaozuru nchini humo watapewa visa pindi tu wanapofika kwenye uwanja wa ndege.

    Sheria hiyo itaanza kutekelezwa mwaka 2018 na inalenga kuongezea urahisi wa kuingia nhini huo na kuungana na nchi zote duniani.

    Wageni wote watapewa visa ya siku 30 na pia watalipia watakapoingia nchini humo.

    Aidha raia wa Rwanda wenye uraia wan chi nyingine wataruhusiwa kuingia nchini humo kwa kutumia vitambulisho vyao.

    Taarifa kutoka kwa mkuu wa uhamiaji inasema raia wan chi kadhaa zikiwemo Benin, , Chad, Ghana, Guinea, Indonesia, Haiti na Senegal, watapewa visa ya siku 90 wanapoingia nchini humo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako