Ripoti iliyotolewa jana na Umoja wa Mataifa imekadiria kuwa, uchumi wa dunia utaongezeka kwa asilimia 3 katika mwaka 2018 na mwaka 2019, ambao umezidi makadirio ya awali, sababu kuu ikiwa ni nguvu kubwa ya ongezeko la uchumi la nchi zilizoendelea na mazingira mazuriya uwekezaji.
Lakini ripoti hiyo pia imeonesha kuwa, hali ya biashara imezidi kuwa na wasiwasi, sera ya fedha imezidi kuyumba, kiwango cha madeni kimeongezeka, na hali ya wasiwasi ya siasa ya kijiografia imezidi kuwa mbaya, mambo yanayoweza kuzuia maendeleo ya uchumi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |