v Nyaraka muhimu zatangazwa baada ya kufungwa kwa Mkutano wa kilele wa FOCAC wa Beijing Mkutano wa kilele wa Baraza la ushirikiano kati ya China na Afrika FOCAC uliofungwa jana hapa Beijing ulitangaza nyaraka mbili muhimu zikiwemo Azimio la Beijing, na Mipango ya utekelezaji, ambazo zimeonesha kwa pande zote maafikiano kati ya China na Afrika kuhusu masuala muhimu duniani kwa hivi sasa. Rais Xi Jinping wa China ameeleza kuwa mkutano wa kilele wa FOCAC wa mwaka huu umefungua ukurasa mpya wa kihistoria wa uhusiano kati ya pande hizo mbili, na kuweka mnara mpya katika ushirikiano kati ya kusini na kusini katika zama mpya.
|
v Mashaka ya nchi za magharibi hayatazuia ushirikiano wenye ufanisi mkubwa kati ya China na Afrika Mkutano wa Baraza la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) unaendelea hapa mjini Beijing. Katika miaka 18 iliyopita tangu kuanzishwa kwa Baraza hilo, kumekuwa na mashaka na kupaka matope ushirikiano kati ya pande hizo mbili, lakini hata hivyo, ushirikiano kati ya China na Afrika umepiga hatua thabiti na kupata matunda mazuri. Wakati huo huo baadhi ya vyombo vya habari vya nchi za magharibi na washauri bingwa ambao walitilia shaka juu ya ushirikiano kati ya pande hizo mbili wametoa ripoti inayoonesha ukweli wa mambo.
|
v Rais Xi Jinping wa China ahutubia ufunguzi wa Mkutano wa kilele wa Beijing wa FOCAC Tarehe 3 Mkutano wa kilele wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika umefunguliwa kwa shangwe kwenye Jumba la mikutano ya umma la Beijing. Rais Xi Jinping wa China alihudhuria ufunguzi wa mkutano na kutoa hotuba isemayo "Tushirikiane kwa kuelekea mustababali wetu wa pamoja na kuhimiza maendeleo kwa moyo mmoja",
|
|