Wachezaji wa rugby watakaoshiriki michuano ya rugby ya kombe la dunia itakayofanyika mwakani nchini Japan wameonywa kutoonyesha michoro ya mwilini yaani tattoo wakiwa kwenye michuano hiyo ili kutowakwaza watu na kuheshimu utamaduni wa kijapani.
Tamko hilo limetolewa na bodi ya mchezo wa rugby nchini humo na kuwataka wachezaji wote kuvaa flana wanapokuwa mazoezini au kwenye mabwawa ya kuogelea.
Timu zote zitakazoshiriki michuano hiyo tayari zimeshapatiwa barua za agizo hilo mapema ili kuepuka faini ama kufungiwa pindi watakapokiuka agizo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |