Mwanasoka Romelu Lukaku ambaye ni raia wa Ubelgiji ameshinda tuzo baada ya kufanikiwa kuingia kwenye orodha ya wachezaji 28 tu kuwahi kufikisha kufunga mabao 100 kwenye ligi kuu ya Uingereza (EPL).
Lukaku amefunga bao lake la 100 mwishoni mwa msimu uliopita katika mechi na Swansea City.
Lukaku amemshukuru aliyekuwa mchezaji bora Didier Drogba kwa ushauri wa kila siku na kuufanyia kazi, huku akisema bado ana kiu ya kutikisa nyavu za wapinzani zaidi na tuzo hiyo haimfanyi kuridhika na kujiona amemaliza kila kitu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |