• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rais wa Rwanda awakaribisha Wachina kutembelea Rwanda

    (GMT+08:00) 2018-11-12 21:08:23

    Rais paul Kagame wa Rwanda ametuma salamu kwa Wachina na kuwakaribisha kutembelea nchi hiyo, wakati mauzo ya punguzo kubwa ya tarehe 11/11 ukianza usiku wa kuamkia jumapili.

    Ujumbe wa rais Kagame kwa soko la China ulirushwa moja kwa moja katika Maonyesho ya 11/11 yaliyofanyika kwenye uwanja wa Mercedes Benz mjini Shanghai. Ujumbe huo pia ulionyesha mandhari ya kuvutia ya Rwanda pamoja na vivutio vingine vya utalii, ikiwemo ngoma ya utamaduni ya Itore.

    Siku hiyo ni ya kipekee nchini Rwanda, kwa kuwa nchi hiyo imeingia mkataba na Kundi la Alibaba ili kuwezesha kupatikana kwa urahisi kwa bidhaa za Rwanda katika soko la China.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako