• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Umoja wa Afrika wazindua mfuko wa kuhimiza amani na usalama

    (GMT+08:00) 2018-11-18 16:59:05
    Umoja wa Afrika umezindua mfuko wenye lengo la kuhimiza amani na usalama barani Afrika. Akiongea kwenye uzinduzi wa mfuko huo, Rais Paul Kagame wa Rwanda ambaye pia ni mwenyekiti wa zamu wa Umoja wa Afrika, amesema mfuko huo utasaidia kuhakikisha changamoto za amani na usalama, zinatatuliwa kwa njia ya kiafrika.

    Akiongea kwenye mkutano wa pembeni kwenye mkutano maalumu wa kilele wa 11 wa Umoja wa Afrika, Rais Kagame amesema mfuko huo utakuwa na bajeti ya kuanzia dola milioni 100 za kimarekani, na mpaka sasa nchi za Afrika zimechangia dola milioni 60 za kimarekani. Rais Kagame amezishukuru nchi 42 wanachama wa AU zilizotoa mchango, na kuzitaka nyingine 12 ambazo bado hazijatoa zifanye hivyo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako