Msemaji wa kamati ya maendeleo na mageuzi ya China Bw. Meng Wei leo hapa Beijing amesema, China itapunguza zaidi vikwazo vya kuingia kwenye soko, na kuruhusu kampuni za kigeni kuwekeza katika sekta nyingi zaidi.
Vilevile, amesema China itaendelea kuboresha mazingira ya kisheria ya uwekezaji, na kuhimiza zaidi ushindani wa usawa. Amesema China itauhimiza ufunguaji mlango katika sekta ya huduma, kufungua mlango zaidi katika sekta za kilimo, uchimbaji wa madini na utengenezaji, kuharakisha mchakato wa kufungua mlango wa sekta za mawasiliano ya habari, elimu, matibabu na utamaduni, pia kupanua zaidi maeneo kwa uwekezaji wa wafanyabiashara wa nchi za nje.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |