• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • RAGA: Lionesses kujaribu bahati kufuzu michuano ya raga ya dunia

    (GMT+08:00) 2019-03-15 07:49:28
    Droo ya mechi za kufuzu kushiriki mchezo wa raga ya dunia ya wachezaji saba kila upande ya wanawake mwaka 2019 imetangazwa, huku Lionesses ya Kenya ikijikuta katika kundi moja na majirani zao Uganda pamoja na Papua New Guinea na wenyeji Hong Kong.

    Michuano ya kufuzu inatarajiwa kufanyika mwezi ujao mjini Hong Kong ambapo mshindi atajikatia tiketi ya kujumuishwa katika duru zote za msimu 2019/2020.

    Kenya itakuwa ikijaribu bahati tena ya kufuzu michuano ya raga ya duniani baada ya kutolewa na Afrika Kusini katika nusu fainali mwaka jana.

    Kundi A lina ti u za Japan, Ubelgiji, Scotland na Mexico ambapo kundi C linajumuisha Brazil, Argentina, Kazakhstan na Poland.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako