Kiongozi wa ujumbe wa China kwenye mkutano wa Baraza la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa ambaye pia ni naibu waziri wa mambo ya nje wa China Bw. Le Yucheng jana huko Geneva alisema kuwa, lengo la China ni kuwezakutokomeza umaskini kwa pande zota ifikapo mwaka 2020 ambalo litakuwa maajabu mapya katika historia ya maendeleo na kupunguza umasikini duniani ni mchango mkubwa wa China kwa mambo ya haki za binadamu duniani.
Bw. Le Yucheng amesema, katika miaka 40 iliyopita, China imewasaidia watu milioni 740 kuondokana na umaskini, na mwaka 2018 imetimiza watu milioni 13.86 kuondoa umaskini.
Bw. Le Yucheng pia alisisitiza kuwa, China siku zote inahimiza maendeleo ya haki za binadamu ya China yanayozingatia watu, na kufanya juhudi ili kutimiza lengo la maisha mazuri ya watu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |