Umoja wa Mataifa umetoa wito kwa pande zote kujizuia kadri ziwezavyo katika mivutano kati ya Iran na Marekani na kwenye eneo la Ghuba. Marekani imeongeza shinikizo dhidi ya Iran kwa kutaja jeshi la walinzi wa mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran kuwa kundi la kigaidi, kupiga marufuku kabisa biashara ya mafuta ya Iran na nchi za nje na pia kutuma wanajeshi kwenye eneo la Ghuba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |