• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • RAGA: Michuano ya Raga ya Dunia U-20- Kenya na Japan zataja vikosi vyao

    (GMT+08:00) 2019-07-18 09:24:02
    Makocha Paul Odera wa Kenya na Yoshite Mizuma wa Japan, wametaja vikosi vyao kabla ya mechi ya raga ya dunia ya wachezaji 15 kila upande ya vijana wasiozidi umri wa miaka 20 itakayopigwa uwanja wa Martins Pereira mjini Sao Paulo nchini Brazil leo.

    Odera amefanya badiliko moja pekee katika kikosi chake ambacho kimepata kupumua baada ya nyota Andrew Siminyu, Jeff Mutuku na Douglas Kahuri kupona majeraha waliyoyapata na kurejea kuitumikia timu hiyo ya Kenya.

    Washindi wa makundi yote mawili watakabiliana katika fainali Julai 21 kuamua timu itakayopandishwa ngazi kushiriki raga ya dunia ya daraja ya juu kabisa (JWC) mwaka 2020.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako