Super Eagles ya Nigeria imefanikiwa kukamata nafasi ya tatu na kuondoka na medali ya shaba baada ya kuifunga Tunisia kwa goli 1-0. Goli lililopachikwa kimiani na Odion Ighalo dakika ya 3 ya mchezo.
Kesho ndio kesho, mafahari wawili, Mbweha wa jangwani Algeria itakapovaana na Simba wa Teranga ya Senegal katika mchezo wa fainali na kuhitimisha mashindano hayo. Ni nani atachukua ubingwa wa Afrika?majibu tutayapata ama baada ya dakika 90, ama dakika 120, am ahata kwa njia ya matuta, lakini kesho lazima kieleweke.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |