Watu zaidi ya 50 wamefariki dunia baada ya treni ya mizigo kuacha njia mkoani Tanganyika, kusini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC. Waziri wa masuala ya kibinadamu Steve Mbikayi amethibitisha habari hiyo na kudokeza kuwa mkutano wa dharura unafanyika ili kupanga mipango ya lazima ya kuwasaidia wahanga. Mitandao mingi ya reli nchini DRC ilijengwa katika kipindi cha ukoloni na haikufanyiwa matengenezo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |