Rais Hassan Rouhani wa Iran amesema Iran inataka kubaki kwenye makubaliano ya nyuklia ya mwaka 2015 ambayo yanalingana na maslahi yake.Rais Rouhani amesema kupitia hatua hiyo, Iran itatimiza lengo kubwa la kisiasa la usalama. Ameongeza kuwa kwa mujibu wa makubaliano hayo, na azimio namba 2231 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, vikwazo vya silaha ilivyowekwa Iran na Umoja wa Mataifa vitaishia mwishoni mwa mwaka ujao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |