Wakati timu ya Simba ikiongoza katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, kocha mkuu wa timu hiyo Patrick Aussems amesema anafurahia kuona ushindani uliopo katika ligi hiyo msimu huu umeongezeka, hivyo kuongeza umakini wa timu yake. Amesema ushindani huo pia umesaidia kuimarisha viwango vya wachezaji kwa sababu kila mmoja anajiimarisha ilia pate namba katika kikosi cha kwanza.