Kagame aliyasema hayo jana jijini Johannesburg,Afrika Kusini,katika makala ya pili ya Mkutano wa Uwekezaji wa Afrika ulioandaliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika.
Rais Kagame alisema wimbi la uwekezaji Afrika haliwezi kupinduliwa kwa kujua tu kipi kinahitajika kufanyika au uwezo lakini ni kwa kukifanya.
Aliwachachawiza viongozi na wadau kutoka sehemu mbalimbali za Afrika kukamata kila fursa inayopatikana ili kufika kule bara hili linapotakikana kufika.
Rais Kagame alizungumza hayo mbele ya Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa,Rais wa Ghana Nana Akufo-Addo,na Waziri Mkuu wa Msumbiji Carlos Agostinho do Rosario katika majadiliano ya jopo kuhusu kuwekeza Afrika.
Mkutano huo wa uwekezaji Afrika ulifunguliwa jana na unatarajiwa kufungwa tarehe 13 mwezi huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |