• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Ni wakati wa Afrika wa uwekezaji-Rais Kagame

    (GMT+08:00) 2019-11-12 19:05:26
    Rais wa Rwanda Paul Kagame amesema bara la Afrika linafaa kukumbatia kila fursa inayopatikana ili kuvutia uwekezaji.

    Kagame aliyasema hayo jana jijini Johannesburg,Afrika Kusini,katika makala ya pili ya Mkutano wa Uwekezaji wa Afrika ulioandaliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika.

    Rais Kagame alisema wimbi la uwekezaji Afrika haliwezi kupinduliwa kwa kujua tu kipi kinahitajika kufanyika au uwezo lakini ni kwa kukifanya.

    Aliwachachawiza viongozi na wadau kutoka sehemu mbalimbali za Afrika kukamata kila fursa inayopatikana ili kufika kule bara hili linapotakikana kufika.

    Rais Kagame alizungumza hayo mbele ya Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa,Rais wa Ghana Nana Akufo-Addo,na Waziri Mkuu wa Msumbiji Carlos Agostinho do Rosario katika majadiliano ya jopo kuhusu kuwekeza Afrika.

    Mkutano huo wa uwekezaji Afrika ulifunguliwa jana na unatarajiwa kufungwa tarehe 13 mwezi huu.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako