Takriban wamiliki wa akaunti za benki 100,000 wataweza kutoa pesa wiki hii,labda kuwe na agizo jingine kutoka Benki kuu ya Zimbabwe.
Gavana wa Benki Kuu ya Zimbabwe Dkt John Mangudya alisema hatua zimechukuliwa kuhakikisha pesa hizo hazitolewi benki na kuingizwa kwenye soko lisilo rasmi la pesa.
Dkt Mangudya alisema anatarajia benki zote kuanza kutoa noti mpya na sarafu hii leo.
Huku viwango vya utoaji pesa vikiwa ni $300 kwa wiki,mamlaka zinalenga kupitia upya viwango hivyo wakati ambapo hali itaimarika,katika juhudi za kurejesha usawa katika uchumi.
Benki pia zinatarajiwa kuanza kuweka pesa katika mitambo ya ATM hivi karibuni.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |