• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • IOM yasema zaidi ya wakimbizi 170,000 wa Afghanistan wamerejea nyumbani hadi sasa

    (GMT+08:00) 2020-01-24 17:01:48

    Shirika la Uhamiaji la Umoja wa Mataifa IOM leo limeripoti kuwa zaidi ya wakimbizi 170,000 wa Afghanistan wamerejea wenyewe nyumbani ama kurejeshwa tangu mwanzoni mwa Januari.

    Kwenye taarifa yake IOM imesema jumla ya Waafghanistan 15,550 wamerejea kutoka Iran, wakiwemo 6,489 waliorudi wenyewe na 9,061 waliorejeshwa. Wakimbizi wa Afghanistan wameripotiwa kukabiliwa na ugumu wa kupata kazi nchini Iran kwa muda mrefu.

    Wakati huohuo Waafghanistan 443 wamerejea kutoka Pakistan na wengine 1,629 wamerejea wakitokea Uturuki bila ya msaada wa IOM, hata hivyo wamesaidiwa na IOM baada ya kuwasili nyumbani. Na wengine 59 wamerejea wakitokea nchi nyingine.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako