Rwanda imetajwa kuwa nchi yenye kiwango cha chini zaidi cha ufisadi Afrika Mashariki na nchi ya nne Afrika kusini mwa Sahara katika ripoti ya Shirika la kimataifa Transparence iliyotolewa jana.
Hata hivyo ripoti hiyo imesema alama ya Rwanda ilishuka hadi 53 kutoka 56 ya mwaka 2019. Mkuu wa mamlaka ya kupambana na ufisadi ya Rwanda Anastase Murekezi amesema nafasi hiyo ya Rwanda inaonesha kuwa hatua za serikali za kupambana na ufisadi bado zinahitajika kuimarishwa.
Wakati huohuo, kwa mujibu wa ripoti hiyo, alama za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zilikuwa 18, Burundi 19, Uganda 28, Kenya 28 na Tanzania 37.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |