• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Misaada ya kukabiliana na Covid 19 yatolewa kwa vituo vya mabasi Tanzania

    (GMT+08:00) 2020-06-12 21:10:18
    Misaada ya kukabiliana na virusi vya Corona imetolewa kwa vituo vya mabasi mkoani Mbezi nchini Tanzania. Msaada huo unatolewa wakati ambapo ujenzi wa kituo cha mabasi ya mkoani Mbezi Mwisho jijini Dar es Salaam, umefika asilimia 79 na unatarajia kukamilika mwaka huu.

    Misaada hiyo ambayo imetolewa na shirika la Wateraid ni pamoja na mashine saba za kunawia mikono na sabuni lita 720.

    Misaada hiyo imekabidhiwa kwa ajili ya kutumiwa katika kituo cha mabasi Ubungo, kituo kikuu cha mabasi yaendayo haraka Gerezani na Kimara Mwisho kwa ajili ya matumizi ya abiria wanaoingia na kutoka katika vituo hivyo.

    Kaimu Meya wa jiji la Dar es Salaam Abdallah Mtinika alisema kituo hicho ni cha kisasa ambacho kitakuwa na mahitaji yote na kwamba serikali ilitoa Sh. bilioni 51 kwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa ajili ya ujenzi wake.

    Ameongeza kuwa kituo hicho kina uwezo wa kuingiza mabasi 700, magari madogo 80 na nje kutakuwa na eneo lenye uwezo wa kupaki magari 1,000.

    Kuhusu msaada waliopokea, aliwataka watumiaji wa vituo hivyo kuzingatia kunawa mikono, ili kujikinga na maambukizo ya virusi vya corona na magonjwa mengine ya kuambukiza.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako