• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Idadi ya watu walioambukizwa virusi vya Corona nchini Marekani yaongezeka kwa karibu 55,000 katika saa 24 zilizopita

    (GMT+08:00) 2020-07-03 19:25:40

    Takwimu kutoka Chuo Kikuu cha Johns Hopkins zinaonesha kuwa idadi ya watu walioambukizwa virusi vya Corona nchini Marekani imeongezeka kwa karibu 55,000 katika saa 24 zilizopita, ambayo ni rekodi mpya ya ongezeko la siku moja.

    Takwimu hizo zinaonesha kuwa idadi ya watu waliothibitishwa kuambukizwa virusi hivyo nchini Marekani imezidi milioni 2.7, na kato yao watu 128,684 wamefariki.

    Mtaalamu wa magonjwa ya kuambukiza nchini Marekani Bw. Anthony Fauci Jumanne alisema, ongezeko la kila siku la watu walioambukizwa linawezekana kufikia 100,000 kama hali ya sasa ya maambukizi haikudhibitiwa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako