• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: Kituo cha mabasi Mbezi Luis chafikia asilimia 80

    (GMT+08:00) 2020-09-18 16:38:13

    Ujenzi wa Kituo cha Mabasi cha Kimataifa cha Mbezi Luis Jijini Dar es Salaam, umekamilika kwa asilimia 80 hii ikimaanisha bado kazi ndogo tu ya kumaliziwa kabla ya kuanza kutumika rasmi na kutoa fursa za ajira mbalimbali na biashara.

    Hayo yameelezwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Abubakar Kunenge alipotembelea kukagua maendeleo ya mradi huo, ambao una lengo la kuongeza ajira kwa vijana wengi huku akibainisha kuwa stendi hiyo imejengwa kutokana na ile ya Ubungo kuzidiwa uwezo, hivyo imekuwa ndogo kulinganisha na mahitaji ya watu.

    Akiwasilisha taarifa ya mradi kwa Mkuu wa Mkoa Kunenge, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Bi. Sipora Liana, alieleza ujenzi wa kituo kipya cha mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani, ni mradi unaogharimu zaidi ya shilingi bilioni 50 za Tanzania, fedha zilizotolewa na serikali kuu kwa ajili ya mradi huo wa kimkakati.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako